what is u repot.png

Nishati mbadala ina maana ya mazingira bora zaidi

Ukosefu wa nishati za kisasa unawaumiza watoto

Kote ulimwenguni, watu wapatao bilioni 1.6 hawana umeme, na watu bilioni 2.4 hawana njia bora za kisasa kwa ajili ya kupika na kupasha joto. Watu wanne kati ya watano wasio na umeme wanaishi katika nchi zinazoendelea na vijijini, hasa Kusini mwa Asia na Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika.

Ukosefu huu wa miundombinu ya kutosha ya nishati huwalazimisha zaidi watu theluthi moja duniani kupika na kupasha nyumba joto kwa kuchoma kuni, kinyesi cha mifugo na mabaki ya mazao. Kaya hizi zinakabiliana na mtihani mgumu: ama wapike kwa kuni nzima na kupata matatizo ya afya, au wasile chakula kilichopikwa.

Moshi majumbani husababisha vifo vya zaidi ya watoto 800,000 kila mwaka. Tabia ya nchi na hali ya hewa vina nafasi katika wingi wa moshi huu katika hewa.

Kuacha kutumia nishati ngumu hadi zile bora—kama vile, gesi, gesi asilia au umeme wa jua—kunaweza kupunguza kwa kiasi kikubwa sana viwango vya uchafuzi wa hewa na wakati huohuo kupunguza madhara ya kimazingira katika uzalishaji nishati na matumizi yake.

Upatikanaji wa huduma za kisasa za nishati kunaongeza upatikanaji wa elimu kwa watoto—hasa wasichana, ambao kwa desturi wao ndio wanaotafuta kuni au vyanzo vingine vya nishati ya kupikia na kupasha nyumba joto.

Ifuatayo